Sunday, March 18, 2018


KAROTI
Karoti ni zao la mizizi ambalo hulimwa zaidi katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro, Iringa, Mbeya na Kagera.
Zao hili hutumika kama kiungo katika mapishi ya vyakula mbalimbali. Huweza kutafunwa mbichi au kuchanganywa kwenye kachumbari. Karoti zina vitamin A, C na madini aina ya chuma.
MAZINGIRA:
Karoti hustawi vizuri kwenye sehemu zenyejoto la wastani (nyuzi joto 15 hadi 27 za Sentigredi).
Kiasi cha mavuno yanayoweza kupatikana na ubora wa karoti, hutegemea sana aina ya udongo. Hivyo karoti hustawi vizuri katika udongo mwepesi, wenye rutuba ya kutosha, kina kirefu na usiotuamisha maji.
AINA:
Kuna aina nyingi za karoti. Zifuatazo ni aina zinazolimwa hapa Tanzania.
· Nantes:
Karoti za Nantes ni ndefu, huvunjika kwa urahisi, zina umbo la kuchongoka na ncha kali. Aina hii hupendwa sana kutafunwa na walaji, kutokana na ladha yake tamu. Karoti za Nantes hazifai kwa kusindikwa.
· Chantenay Red Core
Hizi ni nene kwa umbo, na zenye ncha butu. Unene wa nyama ya nje na ndani hulingana hivyo zinafaa sana kwa kusindikwa.
Huwa na rangi ya machungwa iliyofifia na ladha yake siyo tamu.Aina hii hustawi vizuri kwenye udongo mzito.
· Oxheart:
Karoti za Oxheart ni fupi na nene. Huvunwa baada ya muda mfupi kulinganisha na aina zingine.
· Cape Market:
Aina hii hupendwa sana kutafunwa zikiwa mbichi pia zinafaa kusindikwa.
· Flacoro:
Aina hii huzaa sana na mizizi yake ni mirefu. Hufaa kwa kuhifadhiwa na kusafirishwa, kwa sababu haziharibiki haraka.
· Top Weight:
Aina hii ina sifa kama za Flacoro.

Karoti
KUTAYARISHA SHAMBA
Ili kupata mavuno mengi na bora, eneo la kupanda halina budi kutayarishwa vizuri. Iwapo shamba ni jipya, miti na visiki vyote vikatwe. Visiki na takataka zote ziondolewe shambani. Baada ya hapo shamba lilimwe vizuri na katika kina cha kutosha. Lainisha udongo ili kurahisisha uotaji wa mbegu za karoti ambazo ni ndogo sana.
Kama eneo lina udongo wa mfinyanzi au wa kichanga ni muhimu kuweka mbolea za asili zilizooza vizuri. Mbolea hizi hufanya udongo wa mfinyazi uwe mwepesi wa kuweza kuruhusu maji na hewa kupenya kwa urahisi.
Endapo karoti zitastawishwa wakati wa mvua nyingi zipandwe kwenye matuta yaliyoinuliwa.

KAROTI
Karoti ni zao la mizizi ambalo hulimwa zaidi katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro, Iringa, Mbeya na Kagera.
Zao hili hutumika kama kiungo katika mapishi ya vyakula mbalimbali. Huweza kutafunwa mbichi au kuchanganywa kwenye kachumbari. Karoti zina vitamin A, C na madini aina ya chuma.
MAZINGIRA:
Karoti hustawi vizuri kwenye sehemu zenyejoto la wastani (nyuzi joto 15 hadi 27 za Sentigredi).
Kiasi cha mavuno yanayoweza kupatikana na ubora wa karoti, hutegemea sana aina ya udongo. Hivyo karoti hustawi vizuri katika udongo mwepesi, wenye rutuba ya kutosha, kina kirefu na usiotuamisha maji.
AINA:
Kuna aina nyingi za karoti. Zifuatazo ni aina zinazolimwa hapa Tanzania.
· Nantes:
Karoti za Nantes ni ndefu, huvunjika kwa urahisi, zina umbo la kuchongoka na ncha kali. Aina hii hupendwa sana kutafunwa na walaji, kutokana na ladha yake tamu. Karoti za Nantes hazifai kwa kusindikwa.
· Chantenay Red Core
Hizi ni nene kwa umbo, na zenye ncha butu. Unene wa nyama ya nje na ndani hulingana hivyo zinafaa sana kwa kusindikwa.
Huwa na rangi ya machungwa iliyofifia na ladha yake siyo tamu.Aina hii hustawi vizuri kwenye udongo mzito.
· Oxheart:
Karoti za Oxheart ni fupi na nene. Huvunwa baada ya muda mfupi kulinganisha na aina zingine.
· Cape Market:
Aina hii hupendwa sana kutafunwa zikiwa mbichi pia zinafaa kusindikwa.
· Flacoro:
Aina hii huzaa sana na mizizi yake ni mirefu. Hufaa kwa kuhifadhiwa na kusafirishwa, kwa sababu haziharibiki haraka.
· Top Weight:
Aina hii ina sifa kama za Flacoro.

Karoti
KUTAYARISHA SHAMBA
Ili kupata mavuno mengi na bora, eneo la kupanda halina budi kutayarishwa vizuri. Iwapo shamba ni jipya, miti na visiki vyote vikatwe. Visiki na takataka zote ziondolewe shambani. Baada ya hapo shamba lilimwe vizuri na katika kina cha kutosha. Lainisha udongo ili kurahisisha uotaji wa mbegu za karoti ambazo ni ndogo sana.
Kama eneo lina udongo wa mfinyanzi au wa kichanga ni muhimu kuweka mbolea za asili zilizooza vizuri. Mbolea hizi hufanya udongo wa mfinyazi uwe mwepesi wa kuweza kuruhusu maji na hewa kupenya kwa urahisi.
Endapo karoti zitastawishwa wakati wa mvua nyingi zipandwe kwenye matuta yaliyoinuliwa.
KAROTI
Karoti ni zao la mizizi ambalo hulimwa zaidi katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Morogoro, Iringa, Mbeya na Kagera.
Zao hili hutumika kama kiungo katika mapishi ya vyakula mbalimbali. Huweza kutafunwa mbichi au kuchanganywa kwenye kachumbari. Karoti zina vitamin A, C na madini aina ya chuma.
MAZINGIRA:
Karoti hustawi vizuri kwenye sehemu zenyejoto la wastani (nyuzi joto 15 hadi 27 za Sentigredi).
Kiasi cha mavuno yanayoweza kupatikana na ubora wa karoti, hutegemea sana aina ya udongo. Hivyo karoti hustawi vizuri katika udongo mwepesi, wenye rutuba ya kutosha, kina kirefu na usiotuamisha maji.
AINA:
Kuna aina nyingi za karoti. Zifuatazo ni aina zinazolimwa hapa Tanzania.
· Nantes:
Karoti za Nantes ni ndefu, huvunjika kwa urahisi, zina umbo la kuchongoka na ncha kali. Aina hii hupendwa sana kutafunwa na walaji, kutokana na ladha yake tamu. Karoti za Nantes hazifai kwa kusindikwa.
· Chantenay Red Core
Hizi ni nene kwa umbo, na zenye ncha butu. Unene wa nyama ya nje na ndani hulingana hivyo zinafaa sana kwa kusindikwa.
Huwa na rangi ya machungwa iliyofifia na ladha yake siyo tamu.Aina hii hustawi vizuri kwenye udongo mzito.
· Oxheart:
Karoti za Oxheart ni fupi na nene. Huvunwa baada ya muda mfupi kulinganisha na aina zingine.
· Cape Market:
Aina hii hupendwa sana kutafunwa zikiwa mbichi pia zinafaa kusindikwa.
· Flacoro:
Aina hii huzaa sana na mizizi yake ni mirefu. Hufaa kwa kuhifadhiwa na kusafirishwa, kwa sababu haziharibiki haraka.
· Top Weight:
Aina hii ina sifa kama za Flacoro.

Karoti
KUTAYARISHA SHAMBA
Ili kupata mavuno mengi na bora, eneo la kupanda halina budi kutayarishwa vizuri. Iwapo shamba ni jipya, miti na visiki vyote vikatwe. Visiki na takataka zote ziondolewe shambani. Baada ya hapo shamba lilimwe vizuri na katika kina cha kutosha. Lainisha udongo ili kurahisisha uotaji wa mbegu za karoti ambazo ni ndogo sana.
Kama eneo lina udongo wa mfinyanzi au wa kichanga ni muhimu kuweka mbolea za asili zilizooza vizuri. Mbolea hizi hufanya udongo wa mfinyazi uwe mwepesi wa kuweza kuruhusu maji na hewa kupenya kwa urahisi.
Endapo karoti zitastawishwa wakati wa mvua nyingi zipandwe kwenye matuta yaliyoinuliwa.

0 comments:

Post a Comment